Florah Amon Nkondola (Binti Sayuni)
Msongo wa mawazo ama stress kwa
kiingereza, ni tatizo ambalo kwa bahati mbaya sana limeendelea kuwa kitu
cha kawaida sana kwa wanaadamu katika zama tulizo nazo. Katika miaka
hii tuliyo nayo, ni sahihi kabisa kusema kuwa, takriban wanaadamu wote
walio hai wamekuwa wakikabiliwa na tatizo hili.
Kuna baadhi ya aina za msongo wa
kimawazo, ambazo zinaepukika na nyingine ni ngumu kuziepuka ila unapaswa
kujua jinsi ya kukabiliana na shinikizo la msongo wa mawazo pale
linapokukabili. Hapa ni baadhi tu ya njia zilizo rahisi ambazo unaweza
kuzitumia kukabiliana na hali hii pindi unapojikuta umetumbukia ndani
yake
1. Jifunze kusema “hapana” hii ni katika
mambo yako binafsi au kazi yako, unaitumiaje hii hapana? Unajua
maofisini kuna swala la kupeana vikazi visivyoeleweka hata vimetokea
wapi, yaani hujamaliza hili unaletea jingine hata kama sio kazi yako…
sasa jifunze kukataa hizi kazi zisizo za kwako ili mradi tu mfurahishe
tu. hivyo hivyo vitu vidogo vidogo ndivyo vinavyokuletea msongo wa
mawazo.
2.Jiepushe na watu ambao mara nyingi
wanakusababishia Stress, unajua ukikaa chini na kufikiria utagundua kuna
mtu flani au kundi flani la watu ndo linalokuleta msongo wa mawazo,
sasa kaa nao mbali kabisa.
3. Simamia mazingira yanayokuzunguka.
Mazingira yanakuzunguka yanaweza kuwa sababu ya stress zinazokukumba,
mazingira yapo nayozungumzia mimi hapa? njia unayotumia kwenda kazini au
kurudi nyumbani ina foleni sana? hiyo nayo inawea kuwa sababu ya stress
ulizonazo, lakufanya epuka matumizi ya barabara kwa wakati huo,
mazingira ya soko wakati wakufanya manunuzi ya bidhaa mbali mbali
yanakupa stress? nenda katika supermarket maana kwa kiasi flani kuna
utulivu na hali ya hewa nzuri
4.Epuka Hasira za haraka, kuna ya mambo
yanayohusu dini,siasa au maisha yako binafsi huwa yanakupa msongo wa
mawazo basi jitahidi kuepukana nayo katika mazungumzo yako ya kila siku
kwasababu yatakupa hasira na kukufanya ukasirike na hili hupelekea kuwa
na msongo wa mawazo, ukiingia sehemu ukakuta watu wanaongelea swala hilo
epuka nao ili usiweze kuchangia na kujikuta unaingia katika mgogoro wa
nafsi
5.Tengeneza orodha ya vitu anavyotaka
kufanya sikuhiyo asubuhi tu ukiamka, mara nyingi unapaswa kujua mambo
ambayo ni ya lazima kuyafanya kwa siku ambayo unaianza ili ikifika jioni
usiwe na viporo, katika orodha yako tenganisha orodha hiyo kwa vitu vya
lazima kufanya na vitu vya kawaida ambavyo hata usipovifanya
hazitakuharibia ratiba yako. kujua kipi cha lazima ni moja ya njia kubwa
ya kupunguza msongo wa mawazo.
Naomba niishie hapa kwa leo maana
nimewaonjesha yale ninayoyajua na ambayo nimejifunza, swala la kuondoa
msongo wa mawazo linapaswa kuangaliwa kiundani zaidi maana ni pana sana,
hapa juu nimeongelea kuepuka stress ambazo si za muhimu ila kuna swala
la saikolojia ambalo kwa kadiri siku zinaendelea, tutaligusia.
Unaweza kuungana na mwandishi wa makala hii kupitia ukurasa wake wa Facebook kwa kubonyeza hapa
No comments:
Post a Comment