Pages

Saturday, July 13, 2013

Jitambue Ya Chris Mauki...FAHAMU JINSI YA KUISHUHULIKIA NA KUIPUNGUZA HOFU--Part 1


Hofu na mashaka ndio adui namba moja anayefilisi nguvu au nishati ya mwili wa mwanadamu kwa haraka kuliko kitu kingine chochote kile.  Wengi wameathiriwa katika maisha yao ya kielimu, kiafya, kijamii, kikazi na hata kiuchumi kwasababu ya  hofu au mashaka.

Wengi wameshindwa kufikia malengo na ndoto zao katika Maisha kwasababu ya hofu na mashaka.

Mara tu hofu na mashaka yanapoota ndani ya mtu hudumu kwa muda mrefu huku yakileta uharibifu mkubwa katika nafasi, akili, na maendeleo ya mtu huyo kwa ujumla.  Makala au mada  hii itakuwezesha kufahamu kwa kiasi kikubwa mambo unayoweza kufanya ili kuondokana au kupunguza athari za hofu na mashaka na pia kuweza kutoa msaada kwa yeyote anayepitia tatizo hili kwa wakati fulani.

Hofu ni mjumuiko wa kujali kusiko na  sababu yoyote (unnecessary concern) au kusiko na maana yoyote juu ya nafsi au utu wa mtu.  Tunasema  hakuna sababu wala umuhimu wowote kwa sababu kujali huku kumejengwa katika misingi ifuatavyo
-         Mtu kujali sana au kuweka  mawazo sana katika vitu ambavyo viko nje ya uwezo wake.
-         Mtu kuanza  kusikitikia mambo yajayo badala ya kujipanga na kujiandaa kuyakabili pale  yatakapo wadia.
-         Kuweka msisitizo zaidi katika jambo moja na kuyasahau mengine. Anayehofu hudhani kwamba ikiwa kile anachokiwekea msisitizo kitashindikana, basi kila kitu kitakuwa kimeharibika.
-         Mtu kushindwa kutumainia imani aliyonayo  juu ya ufanisi wa jambo fulani.  Hofu yake katika jambo fulani huizidi imani aliyonayo na kwahivyo  hali ya kushindwa kuonekana  dhahiri zaidi kuliko hali ya kushinda.

Kwasababu hofu hujengwa katika fikra  zisizo na maana wala uhalisi wowote, basi njia ya kuiweza hofu hiyo ni lazima  iwe kwa kutumia fikra zenye maana na uhalisi ili kuushinda uwezo wako wa kufikiri kushindwa.
Yafuatayo yatakusaidia kukuwezesha kupunguza kiwango cha hofu katika Maisha.

1.           Jiulize swali “Je nini kinachoniangamiza?”
Hofu ni kitu kinacho angamiza, tena huangamiza kwa viwango na hatua tofauti.  Ngoja nijaribu kukupa mfano wa maelezo.
Hofu kwa lugha ya kingereza ni “worry” neno “worry” limetokana na lugha ya Kidachi lenye  maana ya “Worgen”.  Maana ya neno “worgen” ukiipeleka moja kwa moja katika lugha ya kingereza humaanisha “strangle”. Maana ya neno “strangle” kwa lugha ya kiswahili ni “Kunyonga kwa kamba”. Sasa yamkini hapa unanielewa kwanini ninasema hofu huua au kuangamiza.

Uzuri ni kwamba, hofu haiangamizi pasipo kutoa tahadhari kabla,  baadhi ya tahadhari zinazotolewa katika mchakato wa kuangamizwa  na hofu ni pamoja na hamaki za mara kwa mara, mvi za mapema, baadhi ua upele fulani wa ngozi, vidonda vya tumbo (ulcers), matatizo ya kukosa usingizi, kuhitaji kwenda haja ndogo mara kwa mara n.k.

Swali hili la “ni nini kinachoniangamiza?” litakuwezesha kujitathmini wewe mwenyewe. Katika kulijibu swali hili utaweza kutathmini kwa kujiuliza kuwa “Ni nini katika maisha yangu ambacho nimekipa kipaumbele zaidi kuliko afya yangu na Maisha yangu?  Maana ya swali hili ni ukweli  kwamba kama unahofu katika jambo fulani maana yake hilo jambo au hicho kitu umekipa umuhimu au uzito usiostahili kuliko maisha yako.  Je ni jambo gani au  kitu gani umekipa umuhimu au uzito usiostahili katika maisha yako.  Je ni kazi yako?,  Je ni elimu yako? Je ni ujenzi wa nyumba?  Je ni kibali kwa watu? Je ni watoto wako au mwenza wako?  Je ni malipo ya mkopo uliouchukua? Kumbuka haitakufaidia wala kukuongezea chochote kwa kujiua ukikiwaza hicho kitu, mwisho wasiku mwenye  hasara ni wewe.

Hata mwisho  kama hautapoteza maisha yako lakini ukadhoofisha afya yako, faida yake nini nini?  Na afya yako ikipotea, nini tena utakifanya kuyanufaisha maisha yako?

Kama hofu yako ni kwenye kupata kibali machoni pa watu wanaokuzunguka, labda ofisini, chuoni, mtaani nk.  Kumbuka kuwa watu hao wala hawatajali au kukukumbuka pale utakapokuwa unaugulia wodini au nyumbani kwako kisa ni magonjwa yanayohusiana na hofu.
Labda mfano huu waweza kukusaidia zaidi kuelewa ninacho maanisha.
 Mtu mmoja kijana alimuuliza swali mwanafalsafa (philosopher) mmoja akisema, “Nini kinachokushangaza sana kwa huyu kiumbe binadamu?”

Mwanafalsafa alijibu “Ninamshangaa sana kiumbe mwanadamu kwa sababu hupoteza afya yake kwa kiasi kikubwa sana  akitafuta pesa, na baadae hutumia pesa yake yote akiitibu au kujaribu kuirejesha afya yake iliyo potea katika hofu za Maisha.  Kwa kuihofia kesho yake, mwanadamu huyu ametumia muda wote wa sasa akijiandaa na hiyo kesho, na matokeo yake, kwa kuichosha sana afya yake ameshindwa kuifurahia leo yake na hata hiyo kesho yenyewe huiona kwa taabu sana” (Mwenye ufahamu na afahamu).

 
1.     Acha kuyapa mawazo yako au mitazamo yako umuhimu usiostahili
Hofu, woga na hamaki za mara kwa mara ni alama kwamba unayapa mawazo, fikira na mitazamo yako umuhimu usiostahili.  Maana yake ni kwamba kila unaloliwaza au kulifikiri unalichukulia kua ni halisi, ingawa maranyingine ukweli ni kwamba unavyowaza sivyo.

Hakuna ukweli wala  uthibitisho kuwa kila unacho kiwazakitatokea.
Hizi twaweza kuziita fikra laini, pale ambapo unadhani kuwa kila unachowaza kitatolea.  Mtu mwenye ukichaa, akiwaza kuwa kuna mtu anataka kumpiga risasi atakimbia huku na huko kujificha. Wakati ukweli ni kwamba hakuna kitu kama hicho. Wewe sio kichaa, kwanini uweke vyote unavyoviwaza  kama vile ni dhahiri? tena hususani vile vitu vibaya?

Tabia sugu nyingi walizonazo watu husababishwa na fikra, vile wanavyowaza.  Usiruhusu mawazo yako yakufanye mtumwa.  Mawazo ya kitaalam yanaonyesha kwamba kama ukiweka  mawazo yako sana katika kitu fulani, inaweza kuishawishi tabia au utendaji wako katika hali  ambayo yaweza kuanza kufanya hofu zako kuanza kuwa kweli. Ni kwasababu hii ndiyo maana, unashauriwa kuweka  mawazo na fikra zako zote kwenye vitu ambvyo ni vya maana.

2.     Usijiogopeshe kwa vitu ambavyo hutokea kwa nadra sana
Njia bora ya kuyatengeneza mawazo yetu yanayofikiri sana juu ya hatari ambazo kutokea kwa nadra sana ni kwa kuwaza kuwa wewe hautakuwepo pale hatari hiyo itakapo tokea katika eneo hilo, na hivyo haitakuathiri.

Kwanini uwaze kwamba wewe  una bahati mbaya  sana na vyote vibaya vitakapotokea vitakukuta wewe tu.  Najua inawezekama  kabisa lakini nafasi za kuwezekana huko ni ndogo sana.  Mfano. Kwanini uwaze kuwa unapotembea msituni peke yako, mti unaweza kukuangukia.  Au unapokukwa kwenye ndege au meli, ajali yaweza kutokea, au hata unapokuwa safarini kwa gari, jiulize mabasi mangapi yametoka kule unakotokea na kufika salama kule unakokwenda bila shida yeyote, wewe je huwezi kuwa mmoja wa waliokuwa salama?

Kuna mambo mengi ya kuogopesha yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku, na kama ukiogopa na kuhofu kila kitu na kutofuata ushauri unaotolewa hapa, basi kila siku utatembea na kuishi kwa hofu tu.

MASIKITIKO:MCHUMBA WA NEY WA MITEGO AANGUKA, MIMBA YACHOROPOKA


Rapper Nay wa Mitego leo anasherehekea siku ya kuzaliwa ya mchumba wake aliyekuwa mjamzito kwa huzuni kubwa baada ya mchumba wake huyo kukipoteza kichanga chao kufuatia kuanguka jana usiku.

“Jana usiku mke wangu alianguka, alifikia tumbo kwahiyo akawa anasikia kizunguzungu nilipompeleka hospitali daktari akasema mtoto amekufa,” Nay
Awali, Nay wa Mitego ameweka picha ya mchumba wake kwenye Instagram akiwa hospitali na kuandika: Happy bday my lv, Mungu akupe maisha marefu na yenye mafanikio tele. Japo imekukuta uko vibaya tumempoteza kijacho bt ni mipango ya mungu, nakupenda sana mke..!! #966# happy bday 2u ma.”

JE WEWE UPO KATIKA KUNDI LIPI KATI YA HAYA? JITAMBUE.


Wataalam wa mambo ya saikolojia na maumbile wamezisoma tabia mbalimbali za

binadamu na hatimaye wamewagawanya
katika makundi makuu manne yenye kategoria kuu mbili. Kategoria hizo ni

1. Introvant: watu wenye uwezo mkubwa kiakili na wanaotafakari mambo kwa kina

hapa kuna makundi mawili
1.Melancolin 2. Fragmetic

2. extrovants: wana uwezo wa kawaida kiakili na hawana tafakari za kina katika mambo yao
Hapa kuna makundi mawili
1. Sanguine 2. Colerick



Na sasa tuangalie tabia za kila kundi na mienendo yao

1.MELANCOLIN
Watu wa kundi hili (females and males) wana sifa zifuatazo
-wana uwezo mkubwa kiakili (high intelligency Quetient)
-ni wagunduzi wa mambo makubwa ya kisayansi
-wanamudu vizuri masomo ya sayansi na hesabu
-ni watu wenye pole pole na wasio na maneno mengi
-wana hisia kali za upendo na ni kundi linalosadikika kuwa na upendo wa dhati
-Wanawajali sana wenzao hasa wanapokuwa katika shida na matatizo(i.e ndio maana hawa huwa waombaji --wanamaombi wazuri sana kiimani)
-Wana huruma sana na hawapendi kuona wengine wakionewa
-Wanajitolea kwa haraka na kwa dhati katika mambo ya wengine
-Huondoa uchungu wao kwa machozi (wakiumizwa hulia haraka, hasa kwa upande wa wanawake/wasichana)
-Hawajiamini kwa mambo wanayoyafanya (hata wakiwa darasanu si wepesi wa kunyoosha vidole ili kujibu maswali)
-Wanahesabu kushindwa kuliko kufanikiwa (mfano akitaka kuanzisha duka; badala ya kuwaza itakuwaje nikipata faida wanawaza itakuwaje kama duka litaibiwa ama kuungua moto, kwa maswali hayo anajikuta hata anafikia katika uamuzi wa kuahirisha uanzishaji wa mradi huo)
-Wakata tamaa wanapokosolewa.
-Wanapenda sana kutiwa moyo kiuhalisia.
-Wanapenda kusoma, kusikiliza, na kusimulia mambo yenye tafakari na uchambuzi wa kina (hawapendi umbea)
-Wanapotoa mawaidha mahubiri ama ushauri wengi(wanaosikiliza) huwa wanaguswa nao na hubadilika haraka kutokana na mawaidha hayo ama ushauri ama mahubiri hayo
-Hawapendi kuvunja taratibu, sheria za eneo husika.
-Wanapenda usafi na mpangilio mzuri wa vitu vyao
-Ni wa vumilivu sana katika hali mbalimbali (mfano wanapoonewa ama kuumizwa)
-Hawapendi kufuatilia mambo ya wengine pasipo sababu za msingi.
-Ni kundi mojawapo linaloathiriwa sana na magonjwa ya mashinikizo kutokana na kuwa wanawaza sana
-Ni wagumu wa kusahau na hiyo imewasababishia kuwa wagumu wa kusamehe
-Wanaumia sana wanapokosea ama kushindwa jambo Fulani
-Wanajeruhika mioyo yao kirahisi (i.e wakiingiwa na pepo wabaya si rahisi kuwatoka kwa sababu ya kutunza uchungu kwa muda mrefu mioyono mwao)
-Wana busara na hekima nyingi
-Ni watu ambao wakiishika imani fulani wanajitahidi kuitimiliza sheria yote.
-Ni wepesi wa kutubia makosa yao na kutubu kwa ajili ya wengine.
-Wana aibu nyingi sana hasa kwa watu wasiowafahamu wala kuzoeana nao
-Ni kundi la watu wanoridhika haraka
-Masikini wengi kiuchumi duniani ni wa kutoka katika kundi hili kutokana na uoga wao wa kuanzisha mambo kwa kuhofia kushindwa
-Watoto wanaozaliwa katika kundi hili inasadikiwa ni wengi huwa na ndoto za kufanikiwa mapema lakini ni wachache mno ambao huweza kutimiliza ndoto zao kutoka na uoga wa kuanzilisha mambo mapya.
-Kundi linalopenda amani na utulivu
-Wanaogopa sana matatizo, vikwazo na changamoto
-Katika familia baba na mama wakiwa melancolin upo uwezekano mkubwa kwa watoto kuharibika maadili kwa sababu hawa melancolin si wepesi wa kuadhibu
-Mara nyingi hupenda kuonesha sura za tabasamu hata kama wapo katika matatizo makubwa
-Hawapendi kumueleza kila mtu mambo yao binafsi
-Ni kundi la watu wenye marafiki wachache
-Wakati mwingine hupenda kujikataa.
-Ni waaminifu na wasema ukweli
-Wanapenda kusaidia wengine kupita hata uwezo wao
-Ni waaminifu sana kwa mambo ya kawaida na yale ya kiimani
-Hawapendi kujionesha mbele ya macho ya watu
-Hawa hawafai kuwa viongozi (si wazuri sana) kwa sababu wanapenda kusikiliza na kutafakari kila wanachoshauriwa hivyo hujikuta kuwa wanayumba kimisimamo. (mfano kama mkurugenzi/mwenyekiti wa eneo Fulani akiwa ni melancolin yafaa sana msaidizi wake awe ni colerick
-kingine kinachowanyima sifa ya kuwa viongozi wazuri ni kutokuwa na uwezo wa kujieleza kwa kujenga hoja zenye ushawishi mkubwa [Musa wa biblia alikuwa ni mmoja ya watu wa kundi hili, alikuwa hajiamini, anakata tama mapema, mlalamishi, asiyeweza kujieleza, licha ya kupewa msaidizi na Mungu bado tabia zake zilimuathiri na akajikuta anakosa nchi ya ahadi-Kaanani]
-Wanauhesabu upendo wa dhati kutokana na mambo wanayofanyiwa na sio kuambiwa (wanafurahia sana vitendo kuliko maneno}
-Kwa upamnde wa wasichana inasemekana kuwa ndio ambao wanasumbuliwa zaidi na maumivu ya hedhi, na kujifungua


Mifano ya watu wa kundi hili: Musa (wa biblia) Yesu Kristo, Bob Marley, Celin Dion


2: FLAGMETIC
-Wana uwezo mkubwa kiakili baada ya melancolin
-Uwezo wao katika utendaji wa mambo inasemekana ni kati ya asilimia moja na sitini
-Ni mabingwa wa kuahirisha mambo (mfano kama akitaka kwenda kupalili shamba, akafika na kukuta kuwa majani ni -machache atabeba zake jembe na kurudi nyumbani hata kama ni msimu wa kupalilia)
-Wanapenda sana kupuuzia mambo ikiwa hawakuyaelewa ama kuyaona kwa macho yao wenyewe
-Hawapendi kukubali ama kusifia mafanikio ya wenzao
-Ni kundi la watu wabishi sana na ambao ni mahiri wa kujenga hoja kwa jambo wanalolitetea
-Katika ushindani hasa wa hoja huwa hawakubali kushindwa kirahisi (anaweza kusema mti ni gari akajenga hoja akazitetea na wote mkakubali hata kama ni kwa shingo upande)
-Mawakili majaji na mahakimu mahiri duniani ni wale wanaotoka katika kundi hili
-Ni watu wanaopenda kutafiti na kufuatilia mambo mbalimbali ndio maana maongezi yao mengi hatawaliwa na mifano na takwimu halisia
-Wanapenda kufuatilia mambo ya wengine pasipo hata msingi wowote (wanapenda sana ushushushu)
-Wapelelezi mahiri hutoka katika kundi hili
-Ni watu wasioumizwa kufanya makosa
-Hawapendi kuwaamini wenzao
-Ni wepesi wa kupokea lakini ni wagumu wa kutoa ama kujitolea kwa mambo mbalimbali
-Wanatafakari mambo kwa kina na kuyatolea uamuzi wa uhakika
-Mapenzi (love affairs) si kitu kinachowaumiza sana (kundi linaloongoza kwa kuwa single na ambalo ni rahisi kukubali talaka pale inapotokea migogoro katika ndoa zao)
-Wanasamehe haraka sana kwa sababu hawajali (they don’t care)
-Ni wagumu wa kuomba msamaha (i.e mara zote hutaka kuonekana kuwa wapo sahihi) ndio maana hupoteza nguvu za Mungu kirahisi (imani zao zikipoa huwa si rahisi sana kuamka)
-Ni wagumu wa kupokea mambo mapya hasa yahusuyo imani na sera, vile vile si rahisi kuachana na imani ama sera walizozipokea
-Si watu wanaojali muda na ratiba
-Ni rahisi kukatisha mahusiano ya aina yeyete pindi wanapogundua kusalitiwa ama kurubuniwa.
-Hawaogopi kumkosoa mtu ama kumuumbua hata kama ni hadharani
-Hawaumizwi na maneno ya watu dhidi yao
-Ni wasuluhishi wazuri wa migogoro ya kijamii na ya kimataifa na wenye ushawishi wa kina (i.e karama ya utele kwa neno la upatanisho ipo kwao)
-Ni kundi linalifanya mambo mengi lakini kwa ufanisi wa wastani
-Ni kundi la watu ambao sio wakereketwa wa masuala ya usafi na unadhifu (i.e kimavazi na kiutaratibu)
-Wakianzisha jambo huweza kuliachia njiani bila kulimaliza na wala wasiumizwe na kukwama huko
-Ni watu wasiopenda vurugu hasa demokrasia ya ushuluhishi wa hoja inapokwama
-Wapo tayari kusalimisha chochote walicho nacho ilimradi wabakie na amani (wanafahamika kama peace makers)
-Watu waliojaa dharau na ambao muda wote huona wao ni bora kuliko wengine katika mambo yote
-Hawapendi kuelekezwa na mara nyingi eidha huwadharau viongozi wao ama hutengeneza mitazamo na hoja za kupinga matendo, kujitolea na maagizo ya viongozi wao.
-Wanapenda kutekeleza maagizo wanayopewa uso kwa uso na sio yale ya jumuia
-Wakiwa viongozi huweza kujikuta wakichukiwa na watu hasa pale watakapoendekeza tabia yao ya kutojali haja na matakwa ya wale wanaowaongoza.


3.SANGUINE
-Wana uwezo wa kawaida kiakili (mara nyingine mdogo)
-Ni wacheshi sana
-Watu walio na maneno mengi na wasiopumzika kuongea
-Wanajisikia raha sana pale wanapokuwa wakiongea na watu wengine wakiwasikiliza
-Wanapenda kuanika mambo yao binafsi mbele ya wengine
-Waigizaji wa kuchekesha wengi ni wakutoka katika kundi hili
-Wanapenda sana kujisifu na kujikweza
-Wanapenda sana kusifiwa hata kwa mambo ambayo hayana uhalisia
-Wanataka sana kuonekana mbele ya watu kwa kila jambo wanalolifanya.
-Wanavipaji vingi vizuri lakini wanahitaji kusifiwa na kuhamasishwa ndipo huvionesha kwa uhakika
-Wana hisi za zima moto (i.e wanahamasika haraka na kusahau haraka. Ikitokea ajali huwa watu wa kwanza kujitokeza eneo la tukio na kuanza kutoa msaada; lakini akiondoka pale anasahau kila kitu na hata kama ametumwa akalete ambulance, anaweza kuanza kufanya shughuli zake nyingine)
-Muda wote wako nadhifu (ni wakereketwa wa masuala ya usafi na unadhifu)
-Wana kiherehere sana.
-Wagumu wa kuelewa na wepesi wa kusahau
-Ni vinyonga katika tabia zao (wanuwezo wa kuigiza tabia zisizo zao kiuhalisia na watu wasiowajua wasiwagundue kirahisi)
-Wanashawishika haraka sana kupokea mambo mapya lakini ni rahisi kuyaacha
-Wasichana wa kundi hili si rahisi kurubuniwa kimapenzi kwa silaha ya ushawishi wa maneno, kwa sababu na wao wana maneno mengi
-Ni kundi linaloathiriwa sana na love affairs (i.e wao ni multiple lovers-ni kawaida kumkuta sanguine akiwa na wapenzi zaidi ya mmoja: __inasemekana kutokana na maneno yao mengi na ufundi wa kuigiza hisia na tabia wavulana wanaume wa kundi hili huwanasa wasichana kirahisi bila kutumia mtaji mkubwa.)
-Wawapo kwenye jamii hukubalika sana hasa kutokana na ucheshi wao na ukarimu walio nao.
-Wanapenda sana kuwasaidia watu ingawa ni kwa kujionesha
-Ni wahamasishaji wakubwa na wenye ushawishi wenye kukubalika kirahisi
-Ni kundi la wainjilisti wanaoongoza kwa kurudisha kondoo wengi kwa Bwana (wengi wana karama za kuhubiri kwa mvuto na ushawishi wa pekee)
-Hawaumii wanapokosolewa, ama wanaposhindwa jambo
-Ni kundi la watu waoga sana (wanajiamini sana kwa maneno lakini kivitendo ni kunguru)
-Si watunzaji wazuri wa siri (waropokaji)
-Wanapenda kujaribu kila jambo linalokuja mbele yao
-Wanaamini kuwa wao ndio watu bora kuliko wengine
-Wanapenda sana kusimulia mambo ya wengine
-Hawana aibu hata mbele ya watu wasiowafahamu wala kuwazoea
-Wanaume wa kundi hili huamini kuwa walizaliwa kwa ajili ya kuwasaidia wanawake
-Ni wavivu wa kufanya kazi, wanapenda sana starehe na anasa na ndoto za kufanikiwa kwa miujiza huwa zimewatawala (wanapenda kuwaza jinsi ya kupata bahati nasibu, kuzawadiwa fedha na hata kuokota fedha ama madini)
-Ni watu wasiojua namna ya kupanga na kuimudu bajeti kwa ustadi)
-Ni watu wa mipango isiyoona mbali (wakurupukaji) (Ministers of emmergency affairs)
-Ni wazuri katika kusifia(i.e wanazikubali kazi za wengine kirahisi na kwa dhati)
-Kutokana na porojo zao hujipatia marafiki wengi na hivyo kuwa maarufu
-Wanapenda kusikiliza na kusoma vitu ambavyo havina uchambuzi wa kina.
Mfano ni Petro mtume wa Biblia: alipenda kujaribu kila kiti (alipomwona Yesu anatembea juu ya maji alitaka na yeye kufanya hivyo) alipenda kufahamu kila kitu (aliuliza habari za siku za mwisho) alipenda kujionesha kuwa ni jasiri (aliahidi kuteswa na Yesu), alikuwa ni muoga sana (alimkana Yesu mara tatu kwa kuhofia kuteswa na wayahudi), alikuwa ni mwinjilisti wa kutumainiwa (alihubiri siku ya Pentekoste), alikuwa ni mwepesi wa kukubali pindi anapokosolewa (alikiri makosa baada ya kuonywa na Paulo juu ya upotoshaji wake wa kuhubiri kuwa hakuna wokovu kwa wasiotahiriwa)



1. COLERICK

-Wana uwezo wa kawaida kiakili
-Ni wa wakali na wakaidi
-Hawana huruma wala unyenyekevu
-Watu wasiopenda kudharauliwa ama kuonewa
-Wanapenda kuwatawala wenzao muda wote
-Ni viongozi kwa asili ya kuzaliwa
-Wanawaza kufanikiwa pekee na wala sio kushindwa
-Watu wasiokata tamaa mapema
-Wanajiamini kupita kiasi
-Hawana uoga ni majasiri sana
-Hisia zao hasa za upendo, mapenzi hazionekani kwa uwazi(hidden emotions)
-Kundi la watu wenye nguvu nyingi
-Ni madikteta
-Hawapendi kabisa kupingwa wala kukosolewa
-Watu wa kulipiza visasi
-Watu wa vitendo kuliko maneno
-Ni waonevu, wanapenda dhuruma na ubabe
-Ni watu wakulazimisha mambo hata kama hayawezekani
-Huwa wanatumiwa sana kwa ajili ya kuzima ghasia, uasi ama kuanzisha jambo lenye upinzani eneo fulani
-Wanafaa sana kuwa viongozi kutokana na uhodari wao wa kuwaongoza watu kwa sera za ushawishi wenye mlengo -wa kiukandamizaji
-Hawajui kubembeleza
-Hawaongei wala kucheka ovyo
-Wanapotenda jambo huwa wanawaza namna ya kunufaika na hata kama akimsaidia mtu anawaza namna ya kurudishiwa hicho alichokitoa
-Ni kundi la watu matajiri sana duniani hasa kutokana na uimara wao katika kuthubutu kutenda mambo na hali zao za kutoogopa hasara
-Si watu wanaopenda suluhu na amani
-Unadhifu na usafi wao ni wa wastani
-Hawapendi starehe kwa wingi
-Ni watu wanaoweza kufurahia mazingira yenye dhiki na shida
-Siku zote huwa wanatafuta kufanya mambo ya kihistoria ili wakumbukwe hata baada ya kufariki
-Wanafurahia kushuhudia na kutazama hadithi, matukio na filamu zilizosheheni ukatili na za kutisha
-Mifano ya watu wa kundi hilo: Idd Amin, Hitler, etc

*SI TABIA ZOTE ZA KUNDI LAZIMA ZIANGUKIE SEHEMU MOJA



MAMBO MUHIMU UNAYOPASWA KUFAHAMU
-Kila mtu amezaliwa na tabia fulani zinazomfanya awe katika kundi fulani
-Huwezi kujibadilisha kundi
-Kujifahamu kundi lako kunakuwezesha kurekebisha madhaifu uliyonayo na kuimarisha mazuri uliyonayo. Pia inakusaidia kuwatambua watu wengine hivyo kuwa makini namna ya kuishi nao
-Inawezekana kabisa kujifahamu upo kundi gani na pia kwa kusoma na kutazama ni rahisi kutambua makundi ya wengine



*NITATAMBUAJE MIMI NI WA KUNDI GANI?
-Watu wengi wana tabia za makundi zaidi ya moja
-Kwa wale tabia zaidi ya asilimia themenini kutoka kundi fulani hao wanaitwa pure (i.e pure sanguine etc)
-Kama una tabia kutoka kundi zaidi ya moja, unaunganisha majina ya makundi mawili yenye tabia nyingi zaidi, unaanza jina la lile lenye asilimia nyingi zaidi
*Mfan
*Mfano: flag-coleick; cole-flagmetic, flag-colerick , sangu-melancolic, melanco-sanguine: etc
Uchambuzi huu umeandaliwa kwa msaada wa vyanzo mbalimbali ikiwemo, vitabu, tovuti, semina, makongamano.

SAIKOLOGIA'''''''''''''ZIJUE TABIA SABA ZAKUEPUKA ILI UWEZE KUFANIKIWA


Kama kuna mtu ambaye amekuwa akisoma makala zangu tangu nilipoanza kuandika na amekuwa akipenda kufanikiwa kimaisha namuomba kwa unyenyekevu, asiwe miongoni mwa watu ambao watakuwa na tabia zifuatzo kwani haweza kufanikiwa kimaisha.
Hufikiri, kusema na kufanya yasiwezekana

Watu wasioweza kufanikiwa hujaa fikra za kutofanikiwa na mara nyingi hulalamikia sana matatizo yao. Wakati mwingine wasioweza kufanikiwa hugeuza mambo mema na kuyafanya yaonekane mabaya, jua likiwaka watalalamika joto, likipoa watalaumu baridi, watalaumu foleni za barabarani, yaani kwao kila jambo wataligeuza na kulipa sababu mbaya. Hata wanaposhindwa kutekeleza jambo hutoa sababu, yote ni kuzilinda fikara zao za kutofanikiwa.
Tabia hii hukua mpaka kufikia hatua wanapowatazama wenzao hudhani kuwa wanawasengenya, kuwafanyia mambo mabaya, kuwasaliti, ilimradi tu ni kuwa kinyume na mambo mema. Watu wa namna hii hata kama watasaidiwa namna gani hugeuza misaada hiyo kuwa ya kujipendekeza na mara nyingi hupuuza wema haraka na kueneza mabaya ya mtu. Lakini pamoja na yote kutokana na fikra zao kuwa za kushindwa watu wa tabia hii hukata tamaa mapema, pale wanapofanya jambo na kuonekana lina ugumu kidogo.
Hutenda kabla ya kufikiri
Tabia ya pili ya watu wasioweza kufanikiwa kimaisha ni hii ya kutenda jambo kabla ya kufikiria. Watu wa aina hii, kuwa wepesi sana kununua vitu barabarani mara tu wanaposhawashiwa na macho au wauzaji. Utakuta mtu bila hata kujiuliza faida za kitu hicho anaamua haraka kukipata. Ataamua kwa haraka kuoa, kuolewa, kukubali kujiingiza katika mapenzi na hata kufanya jambo lo lote bila kujiuliza atanufaika vipi?
Hupenda kuzungumza zaidi ya kusikiliza

Watu ambao wako katika hatari ya kutofanikiwa ni wale ambao daima ni wazuri katika kuzungumza kuliko kusikiliza. Wao huwa ni wajuajia wa kila kitu, hawako tayari kupokea ushauri. Siku zote wanapokuwa kwenye makundi ya watu pengine wajuzi zaidi yao wao huwa hodari kujenga hoja kutetea mambo yao hata kama hayafai. Unaweza kumkuta mtu ni kiongozi wa ngazi za juu, amefanya kosa na watu wote wameona kuwa kakosea lakini mhusika hujiona si mikosaji.
Mtu anapokuwa muongeaji sana huwa mgumu kupokea ushauri wa ye yote, anachoamua yeye hukifanya kwa imani kuwa kinafaa. Ukiwa mtu mwenya tabia ya aina hii huwezi kufanikiwa kabisa katika maisha yako. Watafiti wa masuala ya biashara ulimwengini waliwahi kushauri kuwa mipango mizuri ya kibiashara hutoka kwa watu masikini, ambao walisema hufikiri zaidi namna ya kujikomboa kuliko matajiri wanavyofikiri katika kujiendeleza, hivyo wakasema kama mtu anataka kufanikiwa kibiashara lazima asikilize mawazo ya masikini si kuwapuuza kwa kujiona ni bora zaidi yao.
Hukata tamaa mapema
Watu wanaotaka kufanikiwa huchukulia ushindwa kama hatua ya kuelekea kwenye mafanikio, lakini watu wasioweza kufanikiwa wanapojaribu mara moja au mbili kuvuka kikwazo fulani cha kimaisha na kushindwa hukata tamaa na kutotaka kujaribu tena kusonga mbele. Wanye tabia ya kushindwa kimaisha hawako tayari kudumu na jambo moja linaloonekana kushindikana kwao kwa muda mrefu. Akiona mwanamke ambaye ni mkorofi kidogo, haraka hukimbilia kumwacha na kutafuta mwingine, mara nyingi si watu wavumilivu.
Akijaribu biashara ya vitumbua kwa wiki moja na akaona havinunuliwi, anaaza kupika maadazi, wiki moja baadaye yuko kwenye mihogo, basi ilimradi ni kuhangaika kusikokuwa na tija katika maisha. Ukitaka kuwa mmoja kati ya watu wasiweza kufanikiwa kimaisha, basi jaribu kuishi maisha ya kukata tamaa mapema unapofanya mambo.
Hujaribu kuwarudisha nyuma wengine
Wasioweza kufanikiwa katika maisha huwa na tabia moja ya ajabu ambayo ilianzishwa na Hawa mwanamke anayetajwa katika Kitabu cha Biblia kuwa ni mtu wa kwanza kufanya dhambi. Mwanamke huyu alipodanganywa na nyoka na kuchuma tunda hakutosheka na dhambi zake, bali alimpelekea na mumewe Adamu naye akala. Mara nyingi watu walioshindwa kimaisha kuwa na tabia za kuwashawishi watu wengine wawe kama wao katika mawazo na matendo.
Tabia za watu wa aina hii huwa si za kimaendelezo kwa vile wao hudhani kuwa njia zao ni sahihi na hivyo hujaribu kwa nguvu zao kuwarudisha wengine nyuma ili wawe kama wao. Ni watu wenye wivu wa ‘kijinga’ wakiona mwingine anaendelea katika hiki na kile humpiga vita ili afilisike. Ni wingi wa fitina, uchonganishi. Wenye tabia za kutofanikiwa hudhani kuwa kukwama kwao hutokana na vikwazo vinavyoletwa na wengine. “Kwa sababu jamaa kanikwamisha hiki na kile, nimkwama kwa sababu ya kaka yangu”
Hupoteza muda mwingi
Watu ambao hawawezi kufanikiwa ni wale ambao hupoteza muda mwingi kufanya mambo yasiyokuwa na tija, kwa kuangalia Tv, kusengenya watu, kunywa pombe, kufanya starehe na kutumia muda hovyo kwenye kazi ambazo hazina msaada kwao. Wapo watu mahodari kutembelea kwenye nyumba za wengine na kuongea huko kutwa nzima bila kujali kama muda waliopoteza wangeweza kufanya kazi na kujipatia kipato.
Huchagua mambo rahisi
Wakati mwingine mafanikio huhitaji kufanya kazi ngumu zenye kuchosha, lakini watu wasiokuwa na uwezo wa kufanikiwa wanapoletewa mambo mawilii huwa wepesi zaidi kuchagua jepesi kulifanya. Kama ni kazi, basi zisiwe ngumu sana ziwe nyepesi nyepesi ambazo watazifanya bila jasho. Watu wasiokuwa kwenye njia ya mafanikio hawapendi kujituma, wepesi kuchoka na mara nyingi hupenda sana kufanya kazi kidogo na kulala sana.
Tabia za watu wasioweza kufanikiwa huwa ni za kukwepa kuwajibika. Hata kama kuna mtu anataka kumpatia kitu na akamwambia awahi kesho yake asubuhi, huchelewa kwa vile hawezi kujihimu asubuhi na kuacha raha ya usingizi, wakati mwingine hata akiambiwa asubiri mpaka muda fulani huwa hayuko tayari kusubiri.
Leo naomba niishie hapa, tukutane tena wiki ijayo kwa mada nyingine nzuri zaidi. Kwa mtu mwenye shida tuwasiliane kwa email richmanyota@yahoo.com .

Ludacris Confirms Getting Paid From 2 Chainz' "Based On A T.R.U. Story" & "B.O.A.T.S. II"

Ludacris Confirms Getting Paid From 2 Chainz' "Based On A T.R.U. Story" & "B.O.A.T.S. II"
Ludacris elaborates on role as "profit partner" with 2 Chainz, says he received a check for 2 Chainz' last studio album.
Prior to 2 Chainz’ current success, the rapper was one of many artists signed to Ludacris’ Disturbing Tha Peace (DTP) label as a member of Playaz Circle. While 2 Chainz, who went by the Tity Boi moniker during his DTP days, has left the Ludacris-led label behind, according to Ludacris the two artists still have a working relationship with one another.
2 Chainz was one of a handful of artists discussed during Ludacris’ appearance on Power 105.1’s The Breakfast Club this week. Ludacris went on to express his pride in 2 Chainz and revealed that on top of working with the Based On A T.R.U. Story rapper occasionally, he also receives a percentage of the profits from Chainz’ solo projects.
"I'm extremely proud of him, I'm extremely happy, he works extremely hard, he deserves everything that he gets…We still work together in different capacities at all times,” Luda revealed. “I'm still a profit partner at the end of the day. I just got a check for my album and his.”
Last year, it was reported that 2 Chainz would even assist Ludacris on his Ludaversal album by taking on the role of A&R, picking and choosing beats for the project. As of now, it’s unclear what specific role 2 Chainz will play on Ludacris’ eighth studio album.
Another former DTP artist to be brought up during Ludacris’ interview was Chicago rapper Shawnna. The female emcee appeared on a number of songs with Ludacris including “What’s Your Fantasy” and “Stand Up” and reportedly left the label with no warning.
“I don’t know what happened to Shawnna,” said the rapper. “I’m just keeping it real with that. We was recording, I was in mid-album and I hear on the internet that Shawnna is signed to T-Pain. And I have not talked to Shawnna since.”
Video of Ludacris’ interview with The Breakfast Club can be found below .

ONEAL AND FEZA WAKI JADILI MIPANGO YAO BIG BROTHER AFRICA. BOYFYA HAPA UJISOMEE

about this ad
As the night came to a much-needed end, the Ruby couple set to wed tomorrow, Oneal and Feza, sat in the bath tub discussing their fears and their strategy at this point in the game.

Oneal was telling Feza that he feared that if he were to leave the Ruby House, whether he was Evicted or moved to the Diamond House, he would find it very hard to not think about her. This made his game plan a bit vulnerable in that regard. He told her that she needed to thank Koketso because she had outlined their current relationship by telling him that he had a chance with Feza.

Oneal also told Feza that he really liked her and that he didn’t want to lose her to The Chase and the situation was confusing because whether or not they stay in the same House, there will still be challenges they have to face. “You and me are a team that is beyond us,” he had said passionately.

Feza was obviously confused by her man’s word because he wasn’t necessarily driving to any point but merely stating his fears, concerns and strategy. She told him that wherever he went, she’d go, so sticking together was the way forward for the Tanzanian chick.

You could see it in her eyes, she really likes this dude and is willing to be with him to the very end, especially because no one knows when his end will be, with his Nomination hovering over them. For Feza, the time is now because as much as everyone has their game plan, challenges will always influence them in a good or bad way.

MSHIRIKI WA TZ NANDO AAMBUKIZWA GONJWA LA NANII NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA


In a hushed conversation between Nando and Bimp, Nando narrated how he got infected with an STD after his liason with Selly!
For the past days we have been seeing Nando and Selly who were once an item getting distant and avoiding each other but not knowing what happened between them. Thank God that nothing can be kept secret forever and so we had to know the cause why the two fell out.
Nando disclosed that Selly gave him chlamydia a Sexually Transmitted Disease, but we can’t tell how true this is. However, if we are to go by the Tanzanian’s revelations, it explains why the two are no longer getting along well as it was the case at the beginning.
Nando for the past days has been ill, down in bed and if at all his words are to be believed, they answer the question; “What has he been suffering from?”
The Tanzanian lad and the Ghanaian dame had strong feelings for each other that it didn’t even take them  a day to open the sexual gates and enjoyed each other’s package through the deed. Despite the fact that he enjoyed Selly’s goodies, Nando made it crystal clear that he wasn’t ready for a serious relationship but just wanted to satisfy the hungry Nando in him.
All in all, we are not sure whether it was Selly who gave Nando the STD or he had it before. And there is also a possibility that he was suffering from another disease. But let’s scrutinize this; For Nando to have been sick and seeing doctors for the past days and with Selly mentioning to Oneal that Biggie told her to be using protection (condoms), it explains that she has also been treated for it.
The same Nando also openly called Selly out on her arena failure right before everyone else causing her to run off crying saying they should nominate her out to go home if that is how badly they all feel about her.
Did Selly make a mistake by getting involved with Nando who has only disgraced her every step of the way since then? What is your view on this is issu.

PICHA ZA MTANZANIA ANAYE TEMBEA KWA MGUU KUTOKA MBEYA MPAKA DAR


Anakwambia safari yake ya kutembea kwa mguu kutoka 87.8 Mbeya mpaka Dar es salaam anaiita Uzalendo Tour kuisupport Taifa Stars na anategemea baada ya kuimaliza, watu wengi wataiunga mkono timu ya taifa Taifa Stars.
Anavyotembea kwa sasa anakutana na watu wengi sana na watu wengi wamekua wakimpigia simu baada ya namba yake kutajwa hewani Clouds FM, wengine amekutana nao njiani na wamekua wakimpa vitu mbalimbali vikiwemo viatu na nguo mpya.
Katoka Mbeya saa kumi alfajiri akafika Makambako saa moja na dakika 19 akiwa tayari katembea kilometa 186, akachukua gari mpaka 92.9 Iringa mjini kwa sababu ilikua imeshakua usiku tayari… akachukuliwa na gari la Wambura mdau wa Power Breakfast ya Clouds FM na kumuacha Iringa mjini alikolala mpaka asubuhi na kuianza safari tena.
Anakwambia saa nane kamili alikua anauanza mlima Kitonga na akaumaliza kwenye saa tisa na dakika kadhaa, baada ya hapo alitembea mpaka kitongoji cha mwisho kabla ya kuianza Ruaha kisha akachukua gari mpaka Morogoro mjini kwa sababu ilikua usiku tayari,  ameamkia 88.5 Morogoro mjini na sasa anakuja 88.5 Dar es salaam.

Anasema hii ni idea aliyokua nayo kwa muda mrefu sana lakini akashindwa kuifanya kutokana na kukosa mda ila anamshukuru sana Gerald Hando wa Power Breakfast @Cloudsfm ambae amemsaidia sana kufanikisha hii safari.
Sio sehemu zote anatembea kwa mguu, usiku ukiingia inamlazimu apande gari.

Source:Millard Ayo

How to Send free text messages to mobile phones online



Learn how to send free SMS text messages to your friends, coworkers and family while on a computer online with help from this Butterscotch Tutorial. This a great way to relay a quick message at your desk when a phone call is not convenient or necessary. Cell phone service providers know this too and charge (sometimes hefty) fees for sending text messages. Here are a few tips to avoid fees by sending text messages to cell phones right from your computer.

See Also

Remember to Give Kudos, Tweet, Like, & Share
Subscribe

Join the Discussion



Share Your Thoughts