Pages

Wednesday, July 24, 2013

FIVE SIMPOLE RULES TO BE HAPPY....TARATIBU TANO ZA KUKU FANYA UWE MWENYE FURAHA.

1.free your heart from hatred

2.free your mind from worries

3.live simply

4.give more

5.demand less  expect miracles in life



no one can go back and make a brand new stat

anyone can start from now and make a brand new start endings....
god didn't  promise day without pain laughter without sorrow sun without rain but he did promise strength for the day comfort for the tears and light for the ways


disappointments are like road bumps the slow you down but you enjoy the smooth road  after wards don't stay on the bumps too long move on.



when you feel down because you didn't get what you want just sit tight and be happy because god has thought of something better to give you

when something happens to you good or bad consider what it means.

there's purpose to life's events, to teach you how to laugh more or not  to cry too hard

you cant make someone love you all you can do is be someone who can be loved the rest is up to the person to realize your worth

is better to lose your pride to the one you love than lose the one you love because of pride

we spend too much time looking for the  right person to love when or finding fault with those we already love when instead we should be perfecting the love we give

never abandon an old friend you will never find one who can take  his place friendship is like wine it gets  better us it grows older. when you have something in this five roles you can share what your friends on other social networks.

Jitambue.....SABABU MBOVU ZA KUINGIA KATIKA MAHUSIANO/NDOA (Fahamu kwanini wengi hujuta baada ta muda mfupi)

Lengo la kuingia kwenye ndoa, liwe zuri au liwe baya ndilo litakalotegemeza aina ya maisha yenu katika ndoa hiyo kuwa ya furaha au ya machungu. Baada tu ya kuoana na huyo mtu wako kwa sababu zisizo za msingi, siku, miezi au miaka siyo mingi utaanza kuchoka na kutamani kutoka nje ya hiyo ndoa kwa maana baina yenu hakuna muunganiko wa ndani (emotional attachment) baina ya wanandoa wawili. Na mara nyingi hali hii hupelekea msongo wa mawazo (stress), mfadhaiko wa moyo na kukosa furaha ndani ya ndoa. Na matokeo ya hali hii kumfanya mwanandoa mmoja au wote wawili kuanza kutafuta kutoshelezwa na kuliwazwa nje ya ndoa na hapa vinazaliwa vitu vingine kama uzinzi, kutengana, talaka au magomvi na mifarakano isiyoisha.

Wanandoa wengi hawajui nini wafanye, nini waelewe ili kufanya ndoa yao zifanikiwe. Thamani ya ndoa na jinsi ndoa inavyochukuliwa sikuhizi ni tofauti sana na nyakati za wazazi wetu, na hii imewafanya wengine kujikuta wako wenye ndoa kwasababu mbovu na hivyo ndoa nyingi kuvunjika au kuyumba baada ya muda mfupi tu. Vitu kama kudhamiria, heshima na uaminifu sio vya maana tena siku hizi, sababu watu wanaogopa kuonekana wazamani na washamba.

Mtazamo wa ulimengu juu ya ndoa umeharibiwa na magazeti, luninga na vitabu mbali mbali. Siku hizi kuishi bila ndoa ni kitu cha kawaida, kuwa na mpenzi nje ya ndoa sio kitu cha ajabu tena, mapenzi nje ya ndoa sio ya kushangaza hata kidogo. Kinyume chake ukionekana kuyashangaa haya, jamii itakushangaa wewe kwa jinsi ulivyo nyuma ya wakati. Mambo yamebadilika sana, zamani binti akikutwa bikira wakati anaolewa ilikuwa sifa kwake na familia nzima, siku hizi binti akikutwa bikira atachekwa, na watu kumshangaa wakihisi ana matatizo fulani. Hali kadhalika kwa kijana wa kiume aliyejitunza. Kwa bahati mbaya sana tunaishi katika jamii ya ajabu isiyoamini katika kujitoa kwa kweli na kudhamiria katika mahusiano. Jamii isiyoamini katika uaminifu, na ndiyo maana magomvi mengi hutokea pale simu ya mmoja inapoguswa. Kuwindana na kuchunguzana kumekuwa kawaida, maadili sio jambo la kuzingatiwa tena. Wanandoa wengi ni wale wenye majeraha ya moyoni na walio umizwa, kwa hiyo hutoka nje ya ndoa zao wakitafuta mwingine aliyeumizwa kama wao ili waliwazane.



1. Hofu ya umri kupita na kuzeeka
Wako wengi sana, hususani watu wa wajinsia ya kike ambao wamejikuta wakiwakubali wanaume wa aina yoyote ili mradi tu nao waolewe maana umri wao ulionekana kusonga sana na hofu ya kutoolewa kutanda. Mwanaume anayehusiana na mwanamke mwenye tabia hii huulizwa au kulazimishwa kila siku kwenda kujitambulisha kwa wazazi wa binti au kutangaza ndoa. Ndoa nyingi za aina hii zimeishia kenye talaka na kutengana.

Wako wengine ambao kwasababu wanakiu sana ya kupata watoto na wameogopeshwa sana habari kwamba wana weza wasipate watoto kwa sababu ya umri wao, basi watacheka na kaka yeyote yule ilimradi tu waolewe au wazae naye. Wengine wajinsi hii wamejuta sana baada ya kujikuta kuwa waliyezaa naye hakuwa BABA bali mwanaume tu, tena kirukanjia tu na kwahiyo wanawake hawa wameishia kulea mtoto au watoto wao wenyewe pasipo mzazi wa pili (single parenting), jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linawaathiri watoto wengi. Kwa wale wanaokimbilia kuolewa ili wakazae watoto, kukumbuka kuwa hata huko kwenye ndoa kuna waliokosa watoto.



2. Kuingia katika ndoa/mahusiano kwa lengo la kusaidiwa au kuongeza kiwango cha kiuchumi ulicho nacho.
Hapa wengine wamewageuza wapenzi wao kuwa mitaji au rasilimali ya kuwaondoa wao pamoja na ndugu zao kutoka kwenye umasikini. Kwa kuthibitisha hili wengine wamepewa majina kama BUZI, ATM n.k.

Katika penzi la namna hii hakuna mguso au muunganiko wa kuhisia (intimacy) baina ya wapenzi, bali kinachowaunganisha pekee ni kile kilicho mfukoni au vile vinavyoshikika na kuonekana tu. Athari za penzi la aina hii lina fungua milango mingi kwa wahusika kutokuwa waaminifu na hata kujihusisha na mapenzi nje ya mahusiano yao.


3. Kuingia kwenye ndoa sababu ya mimba au mtoto aliyepatikana kabla ndoa
Lazima kutofautisha kuwa sababu iliyowapelekea kuzaa mtoto siyo itakayowapelekea kuoana. Acha sababu ya kuoana kwenu iwe penzi lenu la dhati na sio mimba au mtoto. Suala hili linahitaji pia wazazi wajue kwamba kitendo cha watoto kupeana mimba au kupata mtoto hakitoshi kuwa sababu ya kuwalazimisha kuoana, maranyingi wazazi wamewalazimisha watoto wao kuingia katika ndoa sababu ya mimba au mtoto na kujikuta wanawaharibia maisha yao mazima. Yanini kujiingiza katika mahusiano yakudumu kisa umempa au umepewa mimba na kuifanya hiyo ndio sababu ya kulazimisha muishi pamoja kama mume na mke wakati kabla ya mimba hiyo hakuna mmoja kati yenu aliyewahi kuwaza kuwa siku mmoja mtakuwa mume na mke, badala yake baada ya kipindi kifupi mnagundua kuwa hakuna penzi baina yenu bali kinacho waunganisha ni mtoto pekee. Maumivu na vikwazo baina yenu vinawadhihirishia wazi kuwa ninyi wawili hamkutakiwa kuwa pamoja bali mmelazimisha tu. Kinacho fuatia hapo ni kufungulia mlango penzi lingine nje au kufanya mkakati wa kusitisha mahusiano yenu ili kuitafuta furaha ya kweli sehemu nyingine.


4. Kulazimika kuingia kwenye ndoa au mahusiano ya kudumu kwasababu ya upweke, (Loneliness).
Mara nyingi mtu anapokuwa peke yake (single) huwaza kuwa ndoa ndiyo inayoweza kuwa utatuzi mkubwa wa matatizo yake. Nakubaliana na ukweli wa maandiko kwamba “Sio vema mtu awe peke yake…” lakini ni vizuri tukijua tofauti iliyopo baina ya kuwa peke yako na upweke. Hivi ni vitu viwili tofauti: kuwa peke yako inamaanisha kukosa mawasiliano au ukaribu na watu wengine, unakuwa kama uliyetengwa (being alone), wakati upweke (loneliness) inahusisha nafsi, akili na hisia (soul, mental and emotions) kuwa pweke au kujihisi kutengwa na hii ni ngumu kuishuhulikia. Ni heri kuwa peke yako (single) kuliko kuwa kwenye ndoa na bado ukajisikia upweke (lonely). Wako wengine waliodhani ndoa ni suluhisho la upweke waliokuwa nao na mara walipoolewa au kuoa, mawasiliano baina yao yakayumba na hivyo kukomaza upweke kwa wote wawili (Not alone but lonely).


5. Kuolewa au kuoa kwasababu ya shinikizo kutoka kwa wazazi, ndugu au marafiki
Shinikizo hizi zaweza kuwa za kihisia au hata kihalisia. Kihisia ni pale ndugu au wazazi wanapokushawishi mara kwa mara kuoa sababu umri wako unaonekana kwenda na wako wazazi wengine husisitiza kuwa wanataka wajukuu (utasikia mzazi anasema unataka nife sijawaona wajukuu zangu?). Hata kama huhisi kulazimishwa lakini kwa kule kurudia rudia kwa kukumbushwa kila siku kunaweka shinikizo ndani yako, kunaathiri hisia zako na kuweza kukupelekea kuingia katika ndoa isiyopangiliwa. Shinikizo la kimwili au kihalisia ni pale wazazi wanopolazimisha watoto wao kuoa au kuolewa na watu fulani kwa sababu tu ni marafiki zao (family friends) au kwa sababu ya kulinda utajiri na matarajio yoyote binafsi. Ndoa nyingi za aina hii zimekuwa kero na dimbwi la maumivu na machozi, baada ya muda kidogo mna jikuta mali mnazo, wazazi wenu wanapatana na kupendana, lakini nyie kama wapenzi ni maadui wakubwa. Jiulizeni mnaingia kwenye mahusiano kwa furaha yenu au ya wazazi wenu?


6. Kuamua kuoa au kuolewa ili kupata uhuru.
Hii hutokea sana kwa wale waliozoea kubanwa sana na wazazi katika kila wafanyacho hususani katika maamuzi. Wengine huzikimbia familia zao maana hazieleweki, hazina mpangilio na hivyo kutamani kutoka ili wakaanzishe zakwao wenyewe. Kinadada na kinakaka wanachoka kuamuliwa na kuwekewa masharti ya kuvaa, kula, kufanya mambo, kutoka na kurudi kwa muda kwahiyo wanadhani ndoa ndio itawachomoa kifungoni hapo. Ninaushahidi wakutosha wa baadhi ya ambao walikimbilia katika mahusiano ili kuwa huru na kwa bahati mbaya waliyoyakuta huko kwenye mahusiano yaliwafanya watamani hali waliyoiacha nyumbani kwao ingawa kwa bahati mbaya wakati huo ‘it was too late’.