Pages

Thursday, July 11, 2013

PREZZO AMPONDA DIAMOND KWA MAJIGAMBO ....AMWITA....



Majigambo ya Diamond kwenye vyombo vya habari kabla ya Tamasha la Matumaini kufanyika kuhusu kumgalagaza Prezzo kwenye show hiyo hayajampendeza Rapcellency na sasa ameamua kujibu.

Prezzo ambaye jina lake halisi ni Jackson Makini alianza kwa kuweka picha ya gazeti inayowaonesha akiwa na Diamond kwenye habari iliyohusu tamasha hilo na kuandika ‘Hahahaha #DomoSeriously????
Rapper huyo hakuishia hapo aliweka picha nyingine ya Diamond na kuandika: “U talkin money or u talkin nonsense au anashindana na ndovu kun***a?

Mwisho alimalizia kwa kujibu tweet ya mtu mmoja aliyemwambia kuwa huyo ni Diamond kwa kuandika: Unfortunately only “diamonds” I know is the ones on ma neck fam.”

Wajue Wanaume 8 waliojaribu na waliokuwa na mahusiano na Beyonce kabla ya Jay Z




jayz_beyonce
Beyonce mwanamke mrembo,wenye kipaji kikubwa na pia anaingiza pesa nyingi sana kwa kazi yake ya uimbaji na nyingine, bila shaka wanaume wengi wanamtamani wangekuwa na uhusiano naye au kumuoa kabisa kama Jay Z alivyofanya. Kwenye interview nyingi anazofanya Beyonce likija swali la kuzungumzia maisha yake ya kimapenzi huwa anasisitiza mwanaume wake wa kwanza kabisa aliyemtoa usichana wake ni Jay Z kitu ambacho watu wengi na waandishi hawakubaliani nacho. Hiyo yote ni kutokana na Beyonce kuwa na historia ya kuwa na uhusiano na wanaume wengine hapo zamani.Hii hapa list ya watu nane waliojaribu na waliowahi kuwa na mahusiano ya wazi au ya siri na Beyonce kabla ya kuwa na Jay Z.
beyonce-lyndell-1
Lyndell Locke, huyu jamaa ndiyo alikuwa mpenzi wa kwanza wa Beyonce. Unaambiwa jamaa alikuwa akimsindikiza Beyonce kwenye mazoezi ya kuimba na kucheza akiwa ndiyo yupo kwenye harakati za kuwa star. Beyonce anasisitiza kwamba pia hajawahi kuwa na uhusiano wa chumbani na huyu jamaa.
camron-4
Cam’Ron, msanii maarufu aliyewahi kutamba na ngoma Oh Boy, alisema kwamba kwasababu walifanya ngoma pamoja na Beyonce na katika mambo yao mengine huko nyuma ya pazia. Beyonce alimpa nafasi ya ku-share chumba kimoja na yeye lakini watu wengi hawaya amini maneno ya Cam’Ron.
justin-timberlake-55th-annual-grammy-awards-02
Justin Timberlake, moja ya marafiki wakubwa wa mume wa Beyonce. Kulikuwa na uvumi kwamba wawili hawa Justin na Beyonce wali-spend usiku mmoja kwenye club na baadaye kufanya vitu vingi. Japokuwa hii habari haikuwa na uthibitisho wowote lakini ilivuma kwa wakati wake.
michael_jackson
Michael Jackson, baada ya Michael Jackson kufariki P.Diddy alitoa story kwamba kuna siku MJ alitaka kwenda kwenye party pamoja na Diddy akiwa na lengo kubwa la kutaka kukutana na Beyonce na kumelezea hisia zake. Duh! Kumbe Michael Jackson sio mkali wa kuchagua style za kucheza na melody tu, hadi wanawake wazuri anajua kuchagua.
mosdef
Mos Def alijaribu kumpata Beyonce akitumia mwanya wa wakati wanafanya kazi ya pamoja na Beyonce kwa ajili ya MTV, lakini juhudi zake ziligonga mwamba.
Sean-Paul-sean-paul-207569_800_600
Sean Paul ; Huyu jamaa ndiyo anasadikiwa sana kuwa na mahusiano ya siri na Beyonce. Kuna muda walikuwa karibu sana na kufanya mambo mengi pamoja hadi baadaye ketengeneza ngoma ya Baby Boy ya Beyonce pamoja. Ukaribu upo hadi leo na unaweza kuona kwamba hadi marafiki wa Beyonce ni marafiki wa Sean Paul, mtu kama Kerry Rowland ambaye ameipendezesha ngoma ya how deep ya Sean Paul. Sean Paul mwenyewe aliwahi kuulizwa kuhusu hii ishu na alikataa katakata.
worst-marques-houston-2004-large-msg-13070570889
Marquise Huston, huyu jamaa aliwahi kuja Tanzania kipindi flani akiwa na mdogo wake Omarion. Jamaa aliwahi kushikilia bango kwamba aliwahi kuwa na uhusiano na Beyonce akiwa na miaka 17. Baada ya muda kidogo Marquise alipiga kimya mwenyewe.
wyclef
Wyclef Jean, jamaa huyu ambaye pia ni producer aliwasaidia sana wakina Beyonce enzi za Destiny Child kwenye ngoma yao ya kwanza. Katika hizo harakati unaambiwa mtu mzima hakuweka juhudi kwenye kuandaa ngoma peke yake bali pia juhudi ziliwekwa kwenye mtego wa kumnasa Beyonce.

kama ilikupita, unaambiwa Obama kateua balozi mpya kuja Tanzania je aliona nini...????



.
.
mwananchi.co.tz wameripoti kwamba Rais wa Marekani Barrack Obama amemteua msaidizi wake wa karibu ambae ni Mark Childress kuwa balozi wa nchi hiyo Tanzania.
Childress ni msaidizi wa Obama katika Ikulu ya Marekani (White House) akiwa Naibu Mkuu wa Utumishi anayeshughulikia mipango katika Serikali ya nchi hiyo na aliwahi kufanya kazi katika Bunge la Seneti.
Obama amefanya uteuzi huo ikiwa ni wiki moja tangu alipohitimisha ziara yake katika nchi tatu za Bara la Afrika, ikiwemo Tanzania.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Marekani ilisema nafasi hiyo inahitaji kuidhinishwa na Bunge la Seneti la nchi hiyo kwa sababu uteuzi wake unaweza kuwa na maana kubwa katika kutekeleza sera za nje za Marekani.
Kuteuliwa kwa Childress kunaashiria kwamba Balozi wa sasa wa Marekani nchini Alfonso Lenhardt anakaribia kumaliza muda wake, awali Childress ambaye aliwahi kuwa msaidizi na msiri wa muda mrefu wa Seneta wa zamani Tom Daschle, alitarajiwa kushika moja ya nyadhifa mbili katika utawala wa Rais Obama ambazo ni Mkuu wa Utumishi katika Idara ya Huduma ya Afya ya Jamii (HHS) au Naibu Mkurugenzi katika Ofisi ya Maboresho ya Afya katika Ikulu ya Marekani.

Kanye West's "Yeezus" Posters Graffitied By James Franco & OthERS

Kanye West's "Yeezus" Posters Graffitied By James Franco & Others
Mister Cartoon and a handful of other artists add their artwork to Kanye West's "Please Add Graffiti" promotional posters.
Actor James Franco and Los Angeles-based tattoo artist Mister Cartoon were just a handful of artists recruited by GQ magazine to add their own artwork to Windy City rapper Kanye West’s Yeezus posters.
Keeping with the minimalistic approach of West’s Yeezus cover art, various “Please Add Graffiti” posters were placed in a handful of major cities including New York City prior to the release of the album in the hopes that passerby’s would create their own artwork.
Along with Franco and Mister Cartoon, GQ also sent posters to ESPO, Curtis Kulig, and Wil Fry, who all added their own graffiti to the Yeezus posters.
Pictures of the re-worked posters created thanks to GQ’s project can be found below.
Released on June 18, Yeezus serves as Kanye West’s sixth studio album and was created with help from Mike Dean, Daft Punk, and a handful of other artists.




JAY-Z PERFORMS "Picasso Baby" For Six Straight Hours

Jay-Z Performs "Picasso Baby" For Six Straight Hours
Jay-Z to use video shot during his art gallery performance for his official "Picasso Baby" music video.
Brooklyn rapper Jay-Z is continuing to push boundaries with the release of his 12th studio album, Magna Carta Holy Grail. Most recently, the Roc Nation founder appeared at New York City’s Pace Gallery yesterday (July 10) to take part in what’s described as a marathon performance of his album cut “Picasso Baby.”
According to Pitchfork.com, Jay-Z performed the record for six hours straight and will use video from the lengthy performance for the official “Picasso Baby” music video.
Among those in attendance at Pace Gallery during Jay’s unique performance were DMV-based emcee and The Gifted crafter Wale and director Judd Apatow.
On the Timbaland-produced “Picasso Baby,” Jay-Z makes reference to a handful of artists both new and old as he raps, “It ain't hard to tell, I'm the new Jean Michel…Leonardo Da Vinci flows, Riccardo Tisci Givenchy clothes.”
As of now it’s unclear when the “Picasso Baby” music video will be released, but video of Jay-Z performing “Picasso Baby” and interacting with fans at Pace Gallery can be found below (via Miss Info).
RELATED: Jay-Z Says The Internet Killed The Album Review


NASSARI APOKELEWA CHIN YA ULINZI MKALI

Kwa ufupi

Nassari ambaye jana alitarajiwa kupokewa na mamia ya wanachama wa chama hicho, baadaye angefanya mkutano wa hadhara jimboni kwake, aliwasili saa 6:00 Uwanja wa Ndege Arusha.


Arusha. Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, amewasili Arusha na kupokelewa na ulinzi mkali wa polisi, kuanzia uwanja wa ndege wa Arusha hadi ofisi yake ya ubunge Arumeru Mashariki.
Nassari ambaye jana alitarajiwa kupokewa na mamia ya wanachama wa chama hicho, baadaye angefanya mkutano wa hadhara jimboni kwake, aliwasili saa 6:00 Uwanja wa Ndege Arusha.
Hata hivyo, polisi ilitangaza kufuta mapokezi na mkutano wake, kwa maelezo kuwa ni kutekeleza uamuzi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec kuzuia shughuli zozote za kisiasa Arusha hadi kukamilika uchaguzi wa madiwani Julai 14, mwaka huu.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas, alisema wamelazimika kuongeza ulinzi na kuzuia mapokezi hayo na mkutano, kwani vingekiuka maagizo ya Nec.
Akizungumza ofisi za Chadema Mkoa wa Arusha jana, Nassari alieleza kushangazwa na ulinzi mkali wa polisi.
“Ulinzi huu umeanzia Dar es Salaam Airport (uwanja wa ndege), nimeshuka Arusha hadi sasa polisi wanarandaranda nje ya ofisi hizi,” alisema Nassari.
Pia, mbunge huyo alieleza kushangazwa na polisi kuweka ulinzi ofisi yake, huku wananchi wenye shida wakishindwa kuzungumza naye kwa uhuru.
Alisema amerejea Arusha salama na sasa amepona yupo tayari kushiriki kama wakala wa uchaguzi mdogo wa Jumapili.
Akizungumzia maandalizi ya uchaguzi mdogo, Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa, alisema chama kimewapanga wabunge wake kadhaa kuwa mawakala.
“Tumeunda vikosi na Godbless Lema (Mbunge Arusha Mjini) atakuwa anaongozwa kikosi cha QS1 hakuna matata,” alisema

WILIFRED LWAKATARE ALAZWA

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare akiwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam, jana, kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya Shingo. 

Posted  Alhamisi,Julai11  2013  saa 15:4 PM
Kwa ufupi
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye wodi ya uchunguzi ya Sewahaji, Lwakatare alisema kuwa anakabiliwa na matatizo ya pingili za shingo na jopo la madaktari linakutana leo kuamua kama afanyiwe upasuaji ama la

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kutokana na matatizo ya shingo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye wodi ya uchunguzi ya Sewahaji, Lwakatare alisema kuwa anakabiliwa na matatizo ya pingili za shingo na jopo la madaktari linakutana leo kuamua kama afanyiwe upasuaji ama la.
“Nilifanyiwa uchunguzi kwa x-ray na madaktari walisema hakuna jinsi zaidi ya upasuaji na kesho (leo) jopo la madaktari linasoma picha za x-ray kuamua aina ya upasuaji...nimegundulika kuharibika pingili ya sita na saba.
“Nilipata ajali mwaka 2008 na nilipona, lakini nilipatwa na kadhia hii baada ya kufikishwa Kituo Kikuu cha Polisi baada ya kukamatwa na zaidi ni kutokana na kulala chini,” alisema Lwakatare akiwa kitandani.
Alisema kuwa aliwahi kuumwa akiwa Gereza la Segerea alikokuwa anashikiliwa kabla ya kuachiwa kwa dhamana na kwamba alihudumiwa.
Alisema tatizo hilo lilijirudia jana asubuhi ambapo alifikishwa hospitali hiyo na kupatiwa kitanda kabla ya kufanyiwa vipimo vya X-ray na kukutwa tatizo hilo ambalo alisema gharama yake ni Sh3.5 milioni.     SOSO mwananchi.

Interpol yamtia mbaroni Alex Massawe

Alex Massawe 
Posted  Alhamisi,Julai11  2013  saa 9:31 AM
Kwa ufupi
Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.

Dar es Salaam. Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe ambaye alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu, amekatwa Dubai, Falme za Kiarabu (UAE).
Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.
Babile alisema hivi sasa walikuwa wanaandaa taratibu za kumrudisha nchini ambako amekuwa akisakwa kwa muda mrefu.
“Ombi la kuleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request), lina hatua ndefu. Unajua kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza ili Massawe aletwe. Kwanza lazima Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe,” alisema Babile.
Alisema Massawe alikamatwa wakati akifanya taratibu za ukaguzi baada ya kuwasili UAE.
Habari zilizofikia gazeti hili mapema kutoka Dubai zilieleza kuwa Massawe alikamatwa na maofisa wa usalama wa UAE kutokana na alama zake za vidole na kuonyesha kuwa alikuwamo kwenye orodha ya watu waliokuwa wanasakwa na Interpol.
Massawe ambaye anamiliki majumba na biashara ya utalii katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe.
“Maofisa wa Usalama wa uwanja wa ndege walimuuliza kuwa wewe ndiye Alex Massawe? Alikana lakini alielezwa kuwa alama za vidole vinaonyesha anaitwa hivyo,” kilidokeza chanzo cha habari hizi kwa simu kutoka Dubai. Hata hivyo, Babile alisema hakuwa na taarifa za Massawe kukutwa na pasi bandia za kusafiria.
Uvumi wa Aprili
Mapema Aprili 27, mwaka huu kulikuwa na habari kwamba Massawe amekamatwa katika mji mmojawapo ulioko katika Pwani ya Afrika Kusini.
Habari hizo za kukamatwa kwa Massawe, ambaye pia hufadhili masuala ya kisiasa na michezo, zilisambaa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ya Facebook, Twitter na Jamii Forum. Kulikuwa kuna mkanganyiko wa taarifa huku wengine wakidai alinaswa akiwa ndani ya boti huko Afrika Kusini, wengine wakidai alikamatwa wakati akijaribu kuingia Msumbiji akitokea Malawi.
Akizungumzia hilo Babile alisema huo ulikuwa ni uzushi na baada ya kuzisikia taarifa hizo walifuatilia katika maeneo aliyohusishwa kukamatwa na kubaini kwamba hapakuwa na ukweli wowote.

LAANA: HII NDIO ILE VIDEO YA NGONO YA WANAFUNZI WA DODOMA.....

Baadhi ya wanafunzi  wa vyuo vikuu mbalimbali mjini Dodoma  wameoza kwa matukio machafu ya ngono..


Uchunguzi wetu umebaini kuwa siyo kila mwanachuo anayepata nafasi hiyo adimu ya kujiunga na elimu ya juu anafanya kile kilichokusudiwa, badala yake wanafanya kinyume kwa kujihusisha na vitendo haramu na hatarishi vya ngono.
Katika uchunguzi wa muda mrefu,  blog hii imefanikiwa kunasa matukio mbalimbali machafu yaliyopitiliza ya vitendo vya ngono  ambapo picha  na video ya ngono   ya  wanafunzi  wanaosoma chuo  kimoja  mjini Dodoma   imenaswa laivu....






Tarehe 20  mwezi huu wa tano,GUMZO blog ilipokea simu kutoka  kwa mdau mmoja  ambaye  aliipasha  juu ya kuwepo kwa mkanda wa ngono  chuoni hapo ambao umerekodiwa  na wanafunzi wa chuo hicho....
 
Hapa walikuwa wakitazama camera ambayo waliitegesha wenyewe
--------------


Baada ya tarifa hiyo, mtandao huu ulimteua mwandishi wetu  mmoja  ambaye alikabidhiwa majukumu ya kuujua ukweli ikiwa ni pamoja na kuipata video  hiyo kwa gharama yoyote kama ushahidi.... 
VIDEO HIYO TUMEIGAWA MARA 6 ILA LEO TUTAKUONJESHA TU NA PART 1 YAKE...

ZITTO KABWE AWATAKA WANANCHI WAGOME KUILIPA KODI YA SIMU YA SH. 1000.....AMEDAI KUWA KODI,,,,,,


Sakata  la  kodi  ya  line  ya  simu  limeendelea  kuwakuna wanasiasa  wetu  ambao  wamekuwa  wakifunguka  kwa  nyakati  mbalimbali  kupitia mitandao  ya  kijamii....

Baada  ya  January  Makamba, Zitto  kabwe  naye  amefunguka  na  kudai  kuwa  kodi  hiyo  ni  batili  na  ilipitishwa  kinyemela  kwa  sababu  ilikuwa  imeshaondolewa....

Huu  ni  ujumbe  wake  aliouweka  katika  account  yake  ya  facebook:


Baada ya  kauli  hiyo,Zitto  Kabwe  aliandamwa  na  maswali  mengi  sana  toka  kwa  wananchi  wakidai  kuwa  "Makamba  alisema  tuwalaumu  ninyi  maana  ninyi  wabunge  ndo  mlibariki  kodi  hii"

Zitto  naye  alishindwa  kulijibu  swali  hilo  na  kuwataka  wananchi  "wachukue  simu  zao, wawapigie  wabunge  wao  wawaulize  ni  kwa  nini  walipitisha  kodi  hii"

 "Anasema  hiyo  kwa  sababu  wabunge  ndio waliopitisha.Wabunge  ndio  wawakilishi  wa  wananchi.Jambo likipita bungeni hao ndio wa kwanza kulaumiwa.Yupo sahihi kabisa.Mpigie mbunge wako simu muulize kwa nini  alikubali au  hakupinga kodi hii"..Hili  ni  jibu  za  Zitto Kabwe

WEMA AKIMBILIA ZANZIBAR KUJIFICHA BAADA YA KUMJERUHI MENEJA



POLISI wapatao sita Jumamosi iliyopita walivamia nyumbani kwa staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu maeneo ya Kijitonyama kwa lengo la kumkamata kufuatia kesi iliyofunguliwa katika Kituo cha Polisi Kawe jijini Dar.

Awali taarifa zilidai kuwa, tuhuma zinazomkabili staa huyo asiyekaukiwa na matukio ni za kumtukana na kumpiga vibao Godluck Kuyumbu ambaye ni meneja wa hoteli moja maarufu jijini Dar.

Baada ya kesi hiyo yenye jalada KW/RB5988/2013 SHAMBULIO kufunguliwa kituoni hapo Julai 6, mwaka huu mishale ya saa 5 asubuhi, maafande hao wakiwemo wa kike wawili wakiwa wamevaa kiraia walifika mtaa anaoishi staa huyo na kuufunga kabla ya kwenda kugonga katika geti la nyumba yake.
Mara baada ya kugonga geti hilo, alitoka mwanaume aliyefahamika kwa jina la Petman, alipoulizwa kuhusu Wema, alijiumauma huku kijasho kikimtoka kabla ya kutoa jibu la kwamba hakuwepo.
Majibu hayo hayakuwaridhisha polisi hao ambapo walilazimika kuzuia kila gari lililokuwa linat

oka getini hapo wakiamini huenda Wema angetolewa kiujanjaujanja.

Hata hivyo, hawakufanikiwa kumuona ndipo walipolazimika kumuita mjumbe wa eneo hilo na kuomba ruhusa ya kuingia ndani kufanya upekuzi lakini hawakumtia mikononi na taarifa zikawa mwanadada huyo yuko Zanzibar.

Maafande hao waliomba namba ya simu ya Wema na walipompigia alisema yuko Zanzibar, kesi hiyo anaijua na atakaporejea atajisalimisha mwenyewe polisi.


SOURCE: GPL

HIKI NDICHO KILICHOJIRI MAHAKAMANI BAADA YA GODBLESS LEMA.....

Wednesday, July 10, 2013 | 8:22 PM



Mbunge wa Arusha mjini Mh.Godbless Lema leo amefikishwa katika mahakama kuu kanda ya Arusha kwa kosa linalomkabili la kutoa maneno ya uchochezi kwa mkuu wa mkoa Arusha..


Tukio lililo tokea mnamo tarehe 24 mwezi wa Aprili katika chuo cha uhasibu Njiro ambapo wanafunzi hao walikuwa wamekusanyika katika eneo hilo wakitaka kuonana mkuu wa mkoa pamoja na RPC ili kuzungumzia usalama chuoni hapo.

Akisomewa  shitaka hilo mahakamani hapo ,wakili wa serikali  Bi. Elianeny Njiro amesema mstakiwa Lema alifika chuoni hapo siku ya tukio na kuongea  maneno kwa kutumia lugha ya uchochezi  kwamba ‘amekuja kama anakwenda kwenye sendoff 


Kauli hiyo ilichochea vurugu  kwa wanafunzi kwa kupelekea wanafunzi hao kurusha mawe, chupa, wakati huo mkuu wa mkoa alipokuwa akitoa hotuba ,hali hiyo ilipelekea uvunjifu wa amani.
 

Aidha tukio hilo linatokana na mauaji ya mwanafunazi Henry Koga aliyefariki  23/4 kwa kuchomwa kisu na watu wasiofahamika na  liliripotiwa polisi ambapo  polisi waliweza kufika  eneo la tukio  na kufanya  upelelezi  ambapo upelezi huo uliendelea na mshtakiwa  kufikishwa mahakamani . 


Katika maelezo hayo wakili wa mshtakiwa bwana Method Kimomogoro alisema maelezo yanayokubalika  na kwamba mshtakiwa tarehe 24/4/2013 alikuwepo chuoni hapo lakini maneno yaliyosalia kwamba alitoa maneno ya uchochezi sio ya kweli.

Hakimu aliyeendesha kesi Bi Devota Msofe alisema shauri la kesi hiyo litatajwa kwa siku tatu mfululizo  ambazo ni tarehe 20,21,22 mwezi wa nane huku kukiwa na mashahidi kwa upande wa serikali ambao ni SSP Gilles Muloto wa polisi arusha,  Inspecta Jane mkaguzi wa polisi arusha ,inspeta Benard nyambanya,PC Godfrey johachimu Wiliamu mahanyi wa polisi, Faraji kasidi  wa chuo cha uhasibu njiro ,John Joseph wa chuo cha uhasibu njiro,Benjamini simkanga wa chuo, na naibu hamidu..


Hata hivyo  mahakama iliridhia na shauri lililotajwa pamoja na mashahidi na dhamana kwa mshtakiwa inaendele